Back to News
Health Alerts 1 min read

WAATHIRIKA WENGI WA MAGONJWA ADIMU WATAJWA KUBEBA MZIGO MKUBWA WA GHARAMA ZA MATIBABU

Published

February 28, 2025

Author

Kilasara Deborah

Views

21

WAATHIRIKA WENGI WA MAGONJWA ADIMU WATAJWA KUBEBA MZIGO MKUBWA WA GHARAMA ZA MATIBABU

Imebainika kuwa waathirika wa magonjwa adimu wanakabiliwa na gharama kubwa za matibabu, hali inayofanya upatikanaji wa tiba kuwa changamoto kubwa kwao na familia zao.

Kwa mujibu wa Prof. Francis Furia, kutoka Chuo cha Sayansi na Tiba Shirikishi Muhimbili (MUHAS) wakati wa maadhimisho ya siku ya magonjwa adimu duniani amefafanua kuwa mgonjwa wa ugonjwa adimu anaweza kuhitaji matibabu ya gharama kubwa kwa muda mrefu, jambo linalofanya baadhi yao kushindwa kuendelea na tiba.

"Sindano moja ya matibabu inagharimu dola 2,000, na mgonjwa anahitaji moja kila wiki. Gharama hizi ni mzigo mzito, lakini kwa mshikamano wetu, tunaweza kuleta mabadiliko na kuhakikisha kila mgonjwa anapata matibabu anayohitaji," alisema Prof. Furia.

Mara nyingi, wagonjwa wanakosa bima ya afya inayoweza kugharamia matibabu yao, na hivyo kulazimika kutegemea michango ya jamii au misaada ya taasisi mbalimbali.

Takwimu za kimataifa zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 80 ya magonjwa adimu husababisha athari mbaya zaidi kwa wananchi wengi wenye kipato cha chini. Kwa kuwa tafiti juu ya magonjwa haya ni chache, dawa nyingi zinazotengenezwa kwa ajili ya tiba huwa na gharama kubwa kutokana na ugumu wa uzalishaji wake.

Share this article

Help spread the word about child healthcare

KD

Written by

Kilasara Deborah

Member of the Paediatric Association of Tanzania, dedicated to advancing child healthcare across the nation.

Stay Updated

Get the latest news on paediatric healthcare, events, and educational opportunities delivered to your inbox.

Contact Us